𝗛𝗔𝗧𝗜 𝗬𝗔 𝗠𝗔𝗞𝗨𝗕𝗔𝗟𝗜𝗔𝗡𝗢 𝗬𝗔 𝗞𝗨𝗪𝗔𝗝𝗘𝗡𝗚𝗘𝗔 𝗨𝗪𝗘𝗭𝗢 𝗪𝗔𝗧𝗨𝗠𝗜𝗦𝗛𝗜 𝗪𝗔 𝗨𝗠𝗠𝗔 𝗪𝗔 𝗧𝗔𝗡𝗭𝗔𝗡𝗜𝗔 𝗡𝗔 𝗞𝗘𝗡𝗬𝗔 𝗬𝗔𝗦𝗔𝗜𝗡𝗜𝗪𝗔

 


Hati ya makubaliano ya mashirikiano ya kuwajengea uwezo watumishi wa umma wa  Tanzania na Kenya  imesainiwa kati ya Dkt. Ernest Francis Mabonesho, Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania, na Prof. Nura Mohamed, Mkurugenzi Mkuu wa Shule ya Serikali Kenya (Kenya School of Government), mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, na Rais wa Kenya, Mhe. Dkt. William Samoei Ruto.

Hafla hiyo imefanyika  Ikulu, Jijini Dar es Salaam, leo tarehe 4 Mei 2026.
Makubaliano haya yanatarajiwa kuleta maendeleo makubwa katika sekta ya utumishi wa umma kwa kuimarisha mafunzo na ufanisi wa watumishi wa umma pamoja na kupanua ushirikiano wa kiutendaji kati ya nchi mbili.

Post a Comment