WANAWAKE KATA YA PANGANI WAMPA KONGOLE MWENYEKITI WA UWT KIBAHA MJI KUWANOA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI
WANAWAKE KATA YA PANGANI WAMPA KONGOLE MWENYEKITI WA UWT KIBAHA MJI KUWANOA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI Na Victor Masangu, Kibaha Baadhi ya wanawake wa (UWT) Kata ya Pangani iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha wamempongeza kwa dhati Mwenyekiti wa UWT Wilaya ya Kibaha mjini Elina Mgonja kwa kuamua kutekeleza aahadi yake kwa vitendo kwa kufanya ziara maalumu kwa lengo la kwenda kutoa mafunzo maalumu kwa ujasiriamali ya kuweza kutengeneza bidhaa za aina mbali mbali ili kuweweza kujikwamua kiuchumi. Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa ziara ya Mwenyekiti huyo wa UWT Wilaya ya Kibaha Mwenyekiti wa UWT Kata ya Pangani Johari Komba amebainisha kwamba wamefarijika sana kupata fursa hiyo ya kupata ujuzi mbali mbali na kufundishwa jinsi ya kutengeneza bidhaa tofauti ikiwemo jinsi ya kutengeneza sabuni pamoja na ubunifu wa batiki. “Kwa kweli sisi kama wanawake wa UWT kata ya Pangani tunapenda kumshukuru kwa dhati Mwenyekiti wetu wa Wilaya mama yeetu Elina Mgonja kwa kuweza kuamua kutekeleza ahadi yake kwa vitendo ya kuja kututembelea katika Kata yatu na haya m…