VIONGOZI WAPYA WA TAPSEA WAAPISHWA, WATAKIWA KUSIMAMIA KATIBA YA CHAMA
VIONGOZI WAPYA WA TAPSEA WAAPISHWA, WATAKIWA KUSIMAMIA KATIBA YA CHAMA
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Viongozi
wapya wa Chama cha Waandishi Waendesha Ofisi Tanzania (TAPSEA)
wameapishwa rasmi jijini Dar es Salaam, huku wakitakiwa kusimamia Katiba
ya chama na kulinda maslahi ya wanachama katika utekelezaji wa majukumu
yao. Akizungumza
wakati wa kuwaapisha viongozi hao, Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya
Hakimu Mkazi Kisutu, Franco Kiswaga, aliwataka kuzingatia Katiba ya
TAPSEA na kuitumia kama mwongozo katika uongozi wao ili kuhakikisha
wanachama wanaongozwa kwa haki na ufanisi. Kiswaga
amesema TAPSEA ni chama kikubwa chenye wajibu wa kuwatumikia wanachama
wake, hivyo viongozi wanapaswa kuwa imara katika kusimamia maslahi yao
na kuhakikisha chama kinaendelea kusonga mbele. “Niwaombe viongozi mnapotoka hapa mkasimamie vyema Katiba yenu ili kuweza kuondoa migogoro itakayojitokeza,” alisema Kiswaga. Kwa
upande wake, Mwenyekiti wa Taifa wa TAPSEA, Leah Mwamba, aliwashukuru
wanachama kwa kumpa dhamana ya kuwaongoza na kuahidi kushirikiana nao
katika kuh…