MALIMA AFUNGUA TAMASHA LA UTAMADUNI KITAIFA, AWATAKA WATANZANIA KUTUMIA AFCON KUTANGAZA TAMADUNI KAMA VIVUTIO ADIMU

MALIMA AFUNGUA TAMASHA LA UTAMADUNI KITAIFA, AWATAKA WATANZANIA KUTUMIA AFCON KUTANGAZA TAMADUNI KAMA VIVUTIO ADIMU
Farida Mangube Morogoro  Serikali imewataka watanzania   kuitumia vizuri fursa  ya Tanzania kuwa mwenyeji  wa  mashindano ya AFCON 2027 kwa kutangaza   tamaduni za makabila mbalimbali  kama sehemu ya vivitio adimu vinavyopatikananchini humo  sambamba na  kufanya vizuri kwenye michezo hiyo. Kauli hiyo Imetolewa na  Mkuu wa Mkoa  Morogoro,Adam Malima  wakati akifungua Tamasha la Nne la Kitaifa la Utamaduni linalofanyika mjini Morogoro  ambapo jumla ya wahiriki 150,000 kutoka mikoa mbalimbali wanaonyesha  tamaduni.zao. Amesema katika michuano hiyo  licha ya Tanzania kushiriki nchi zingine ni Kenya na Uganda ambazo  zinaendelea na maandalizi ya michezo  hiyo ambapo kwa Tanzania itafanyika Arusha,Dar es salaam na Zanzibar. Aidha amewataka watanzania kuendelea kuheshimu utamadani kwani bila kuwepo Kwa  utamaduni huwezi kuwa na  heshima. Naye  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Gerson Msigwa amesema tamasha Hilo la Kitaifa la Utamaduni lilianzia Mkoani Dar Salaam,likaenda …