WANAFUNZI MUHAS WABUNI TEKNOLOJIA YA KISASA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA
WANAFUNZI MUHAS WABUNI TEKNOLOJIA YA KISASA KUIMARISHA SEKTA YA AFYA Mgunduzi wa Kifaa Cha SIKU SMART, Mwanafunzi wa udaktari mwaka wa tano Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Cauthary R. Abdallah, akizungumza leo Februari 24, 2026 jijini Dar es Salaam kuhusu umuhimu wa teknolojia ya SIKU SMART ambayo imelenga kuwasaidia wanawake kufuatilia mzunguko wa hedhi kwa usahihi wakati wa Maonesho ya Pili ya Ubunifu ya MUHAS (Innovation Week 2026) yaliyofanyika chuoni hapo. Mwanafunzi wa Shahada ya Uhandisi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHAS) Tiba, Bw. Revocatus M. Lazaro (kulia) akieleza umuhimu wa teknolojia ya Pawakit v1.1 katika kufuatilia utendaji wa vifaa tiba hospitalini. Picha ya teknolojia ya SIKU SMART ………….. NA NOEL RUKANUGA, DAR ES SALAAM Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi Muhimbili (MUHA) wamefanikiwa kubuni teknolojia za kisasa zitakazoboreshа sekta ya afya, zikiwemo Pawakit v1.1 na SIKU SMART. Akizungumza Februari 24, 2026 jijini Dar es Salaam wakati wa Maonesho ya Pili ya Ubunif…