VIJANA WATAKIWA KUTUMIA MAJUKWAA YA MAFUNZO KUFUNGUA FURSA ZA KIUCHUMI
Mkurugenzi Mkuu wa Shirika lisilo la kiserikali la Smarticents , Klein August akizungumza kwenye jukwaa hilo jijini Arusha …………… Na Happy Lazaro, Arusha Vijana nchini wametakiwa kutumia majukwaa ya mafunzo, semina na mijadala mbalimbali kama fursa ya kujifunza, kujenga mitandao na kutafuta njia mpya za kujikwamua kiuchumi. Hayo yamesemwa jijiji Arusha na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika lisilo la kiserikali la Smarticents , Klein August wakati akizungumza katika Jukwaa la Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Mkoa wa Arusha, lililowakutanisha viongozi wa Serikali, mashirika ya kiraia na wadau wa maendeleo kujadili nafasi ya NGOs katika maendeleo ya kijamii na kiuchumi. Klein amesema shirika hilo limejikita katika kutoa elimu ya fedha kwa vijana pamoja na makundi maalumu katika jamii, huku ikiendesha mafunzo ya ujasiriamali kwa wajasiriamali wadogo na wa kati kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kusimamia shughuli zao na kuongeza kipato. Amesema kuwa, ushiriki wake katika tukio hilo umempa nafasi ya…