STAMICO YASAINI MKATABA MNONO NA CHUO CHA MAFUNZO (ZANZIBAR )ZNZ

STAMICO YASAINI MKATABA MNONO NA CHUO CHA MAFUNZO (ZANZIBAR )ZNZ
Shirika la Madini la Taifa ( STAMICO) katika muendelezo  wa kuhakikisha linaendelea kuwa kinara  katika kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi Tanzania nzima, leo tarehe 11/8/2026  imeingia mkataba mnono  wa pande tatu kati ya  STAMICO, Chuo cha Mafunzo  na taasisi ya FDH  ya kuhakikisha magereza yote ya Zanzibar  yanaanza kutumia Nishati ya Rafiki  Briquettes. Makubaliano hayo yamefanyika katika ukumbi wa Chuo cha Mafunzo Zanzibar  na kushuhudiwa  na Kamishna  wa Magereza  Zanzibar Khamis Abdalah Khamis pamoja na  Mkurugenzi  Mtendaji  wa STAMICO  Dkt Venance  Mwasse na  Mkurugenzi  wa FDH  Bwn Michael Salali. Akiongea katika hafla hiyo, Dkt Mwasse ameipongeza  taasisi ya FDH kwa kufanikisha kuingia makubaliano  haya ambayo yatawezesha Magereza  zote za Zanzibar  kupata Nishati hii ya Rafiki Briquettes  ambayo  inaenda kuleta afueni kwenye  gharama za Nishati kwa Magereza   lakini pia kuanza kutekeleza agenda ya Nishati Safi kwa taasisi zote zinazohudumia watu zaidi ya 100. "Suala la…