MCHENGERWA ATEMA CHECHE NZITO UFUNGUZI WA MAFUNZO YA MADIWANI WA CCM PWANI
MCHENGERWA ATEMA CHECHE NZITO UFUNGUZI WA MAFUNZO YA MADIWANI WA CCM PWANI Na Victor Masangu, Kibaha Madiwani wa chama cha mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani wametakiwa kujenga mising imara iya kuwa na uzalendo na Taifa lao ikiwa pamoja na kuweka mikakati kabambe ya kupambana na kero na chanagamoto mbali mbali za wananchi ili kuweza kuzitafuta ufumbuzi. Hayo yamebainishwa na Mjumbe wa halmashauri kuu ya (CCM) Taifa Mohamed Mchengerwa (MNEC) ambaye pia ni Waziri wa afya wakati wa kufungua mafunzo maalumu kwa madiwani wa CCM Mkoa wa Pwani ambayo yamefanyika katika shule ya uongozi ya Mwalimu Julias Nyerere iliyopo eneo la kwa mfipa katika Halmashauri ya Manispaa ya Kibaha Mkoa wa Pwani. Mchengerwa amesema kwamba mafunzo hayo kwa madiwani wa Mkoa wa Pwani watawajengea uwezo mkubwa katika suala zima la kuwatumikia wananchi wao ikiwemo kusikiliza kero na changamotto mbali mbali ambazo zinawakabili wanapaswa kuwa wazalendo. Kadhalika Mchengerwa amesema kwamba madiwani wanapaswa kuabdilika na kuwa mstari wa mbele katika kwenda kuwa suluhisho katika kuwas…