HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA YA ROYAL KUFUNGULIWA RASMI MWANZA MEI 10, 2026 'MSAADA MKUBWA KWA KANDA YA ZIWA'
HOSPITALI YA RUFAA YA KANDA YA ROYAL KUFUNGULIWA RASMI MWANZA MEI 10, 2026 'MSAADA MKUBWA KWA KANDA YA ZIWA'
Na Edwin Soko, Mwanza. Kesho Mei 10, 2026 rasmi Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Royal itafunguliwa na kutoa nafasi ya watanzania hususani wakazi wa Kanda ya Ziwa kunufaika na huduma bora na za kisasa za afya. Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Rev. Dr . Barnabas W. Mtokambali Ujio wa Hospital hiyo ya Rufaa ya Kanda unataraji kuwa ni mkombozi mkubwa kwa wakazi wa Kanda ya Ziwa ambao walisubiri kwa muda mrefu na kesho watashiriki kwenye ufunguzi huo kwa shauku kubwa . Afisa Mtendaji Mkuu wa Hospitali ya Royal Dkt. Lusako Mwaikasu alisema kuwa, Shughuli zote za maandalizi ya ufunguzi hapo kesho zimekamilika na wageni mbalimbali wa kutoka ndani na nje ya Nchi wamewasili tayari Jijini Mwanza. Naye Mkurugenzi Mtendaji Dkt. Glory Simon amewahakikishia watanzania kuwa, Hospitali ya Rufaa ya Royal itafanya kazi kwa ufanisi mkubwa hivyo watanzania wategemee kunufaika na huduma bora za afya. Naye Bwana Richard Nickson wa Ghana Jijini Mwanza amesema kuwa, wana Mwanza na Kanda ya Ziwa kwa ujumla wamepokea kwa …