WIZARA YA KATIBA NA SHERIA YATOA MAFUNZO USULUHISHI WA NDOA MKOANI KAGERA

WIZARA YA KATIBA NA SHERIA YATOA MAFUNZO USULUHISHI WA NDOA MKOANI KAGERA
Na  Diana Byera, Bukoba  WIZARA ya Katiba na Sheria imeanza kutoa mafunzo kwa wajumbe wa bodi za usuluhishi wa migogoro ya ndoa, kutokana na ongezeko la kesi za talaka nchini,  Akifungua mafunzo hayo Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya Katiba na Sheria  Franklin Rwezimula  amesema mafunzo hayo yameanzia mkoani Kagera kwa  lengo la kuongeza weledi na mbinu mpya za  usuluhishi wa ndoa katika jamii ili kujenga familia bora na jamii yenye mshikamano  “Takwimu zinaonyesha talaka zilizosajiliwa mwaka 2023 zilikuwa  711,  mwaka 2024  zikapanda hadi 1,569, na  mwaka 2025 talaka  zilizosajiliwa zilikuwa 1,172 na hizo ni zile talaka tu zilitoleawa taarifa na ndoa nyingine zimekuwa zikivunjika kimya kimya  bila kutolewa taaarifa na kuhatarisha   ustawi wa familia na jamii kwa ujumla.” Amefafanua bodi za usuluhishi zinapaswa kufanya kazi kwa weledi na kujiepusha kuwa mahakimu huku akidai bodi hizo zisiwe sehemu ya kupokea rushwa  Bali zijikite kuondomitafaruku  kutovujisha Siri na Kutenda haki. Kwa upande …