Posts

Mradi wa CERA kutafiti mbegu za Mpunga unaohimili Mabadiliko ya tabianchi Afrika.

Mradi wa CERA kutafiti mbegu za Mpunga unaohimili Mabadiliko ya tabianchi Afrika.
Na: Calvin Gwabara – Morogoro. Wakulima wa kilimo cha mpunga kinachotegemea mvua nchini wamewashukuru watafiti wa Mradi wa Mpunga Himilivu kwa Mabadiliko ya Tabianchi na Rafiki kwa Mazingira barani Afrika (CERA) kwa jitihada walizozianzisha kuzalisha mbegu bora ya mpunga unaohimili changamoto za hali ya hewa ili kuinua kipato cha wakulima wa zao hilo Afrika. Hayo yamebainishwa na wakulima kutoka mikoa ya Morogoro, Shinyanga na Songwe wakati wa zoezi la ukusanyaji wa takwimu za awali na taarifa mbalimbali muhimu zitakazosaidia watafiti hao kuweza kujua changamoto wanazokabiliana nazo katika kilimo hicho ili kuweza kusaidia wao kuzalisha mbegu mpya zilizoboreshwa ambazo zitaweza kuhimili mabadiliko hayo ya tabia nchi. Ukusanyaji huo wa takwimu umefanyika kwa ushirikiano kati ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), katika vijiji nane ukishirikisha wakulima wapatao 258. Akizungumza na watafiti hao mkulima Bwana Maroja Shana kutoka Kijiji ch…