Kutembelea wagonjwa ni fursa ya kuelewa shida za wananchi - OMO

Kutembelea wagonjwa ni fursa ya kuelewa shida za wananchi - OMO
Mwenyekiti wa Taifa wa chama cha ACT Wazalendo Mhe. Othman Masoud Othman, amesema kwamba ziara za kuwatembelea wagonjwa na wenye shida katika kipindi cha mwezi mtufufu wa ramadhani ni fursa muhimu kwa viongozi kutambua kwamba wanadhamana kubwa kwa wananchi kuzielewa shida na matatizo waliyonayo na kutafuta namna sahihi ya kuyakabili. Mhe. Othman ameyasema hayo huko Milimani Kiembe Samaki wilya ya Magharib B alipofanya majumuisho baada ya kukamilisha ziara ya kutembelea wagonjwa ndani ya Wilaya ya Magharib A na B akiwa katika siku ya tatu ya mfululizo wa ziara zake za aina hiyo katika kisiwa cha Unguja. Mhe. Othman ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mstaafu, amesema kwamba wananchi wanayo matatizo na shida nyingi ambapo kupitia ziara kama hizo viongozi wataweza kuzitambua kwa urahisi kwa kufika mwenyewe kwenye maeneo yao wanayoishi wananchi. Amesema ndani ya kipindi cha miaka mitano yakuendeleza ziara hizo amepata uzoefu mkubwa pamoja na kujifunza mambo mengi kutoka kwa wan…